MSIBA; MARANGU-KILIMANJARO


Hivi karibuni Mpini Wa Shoka ulisafiri hadi Marangu mkoani Kilimanjaro; Kaskazini mwa Tanzania na kushiriki safari ya mwisho  hapa duniani (mazishi) ya mpendwa wetu, rafiki yetu, ndugu yetu, dada yetu, mama yetu Caides Mature aliyefariki siku ya Jumatatu tarehe 22/04/2013 katika hospitali ya Seliani jijini Arusha. Mwili wa marehemu ulisafirishwa kutoka hospitali ya Seliani kwenda Marangu-kwa mazishi siku ya Jumamosi tarehe 27/04/2013 na kuzikwa siku hiyohiyo nyumbani kwao Marangu-Samanga (ujombani-kwa ukoo wa Mawalla). Ameacha familia ya watoto kadhaa. Poleni sana ukoo wa Mawalla (ujombani) pamoja na ukoo wa Mosha (upande wa baba.)




Baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wa karibu wakiwa wamevalia fulana zenye picha ya marehemu Caides Mature.




Makundi ya watu kutoka pande mbalimbali za Tanzania na hata nje ya nchi, yakiwasili eneo la msiba, Marangu-Samanga.




Wale waliowahi kufika wakiwa tayari wamejituliza kwenye viti wakiifuatilia ratiba ya mazishi.

 

 

Ama, Kwa hakika, sisi sote ni wa Mwenyezi Mungu, na sote kwake tutarejea tu, kwa maana hiyo ni ahadi yake thabiti isiyoweza kamwe kubadilishwa wala kugeuzwa na yeyote yule kwamba, kila nafsi(kila chenye uhai) ni lazima kitayaonja mauti. 

 

Basi na wewe unapofanikiwa kuyahudhuria mazishi ya mwenzio kama hivi, ni fursa nzuri ya kuihoji nafsi yako, "je wakati na wewe utakapofikwa na umauti na kufanyiwa shughuli kama hii, nafasi yako mbele ya yule aliyekuumba unayekwenda kwake ni ipi? Maisha yako ya kila siku hapa duniani yanayo heri yoyote ile itakayokufanya uwe salama mbele zake?" Anza sasa kujitathmini. 





No comments: