UNAIKUMBUKA VEMA NAFSI YAKO?

Kila mara Mpini Wa Shoka kwa hakika umekuwa ukikukumbusha juu ya kuikumbuka nafsi yako, kabla ya dakika yako ya kifo haijakufikia kwa ghafla wakati ukiwa bado haujajiandaa kwa lolote lile la maana la kujisaidia na kujitetea mbele ya yule aliyekuumba, Mwenyezi Mungu. Jana mchana Mpini Wa Shoka ulikuwa kwenye makaburi ya Njiro, nje kidogo ya Jiji la Arusha, kwenye mojawapo ya mazishi yaliyokuwa yakifanyika kwenye viwanja vya makaburi haya…

 Umati wa watu uliohudhuria ulikuwa ni mkubwa mno….




Hata vyombo vya usafiri vilivyousindikiza mwili wa marehemu vilikuwa ni vingi, vikiwa vimeyabeba makundi makubwa ya wasindikizaji, wakiwemo ndugu, jamaa na marafiki…





Haya ni sehemu ya makaburi ya muda mrefu ambayo baadhi yake bado yamesaliwa na mashada ya maua kwa juu yake…



 

Hiki siyo kibanda cha wavu; wala siyo mtambo wa aina yoyote ile. Hili ni mojawapo ya makaburi yaliyojengewa na kuzungushiwa urembo pamoja na uzio.

 

 


Hili ndilo kaburi alimolazwa marehemu (dada) niliyefika kuhudhuria mazishi yake, ambapo baadhi ya ndugu na jamaa waliamua wapate japo picha tu za ukumbusho.





Haijalishi umri! Na wengine pia ndipo wakapata fursa ya kupiga picha kwenye makaburi ya ndugu na jamaa zao waliozikwa siku, miezi au miaka mingi iliyopita.

 

 

Rafiki ndugu yangu, hebu sikia japo kidogo maneno haya ya Mpini Wa Shoka: Kama mwenyewe Mungu aliyeumba kila kitu kinachoonekana kwa macho na hata vile visivyoonekana kabisa, ndiye aliyeahidi kwamba kila chenye nafsi ni lazima kitaonja umauti, ni kwa vipi wewe unajipumbaza na kujizuibaisha tu na mambo ya dunia hii na hasa yale yasiyompendeza wala kumvutia kamwe huyo aliyekuumba, wakati ahadi yako iko wazi tu ndani ya ahadi yake! Acha kujidanganya; jitambue mapema kuanzia sasa, kabla sekunde ya ahadi yako haijakufikia kwa ghafla tu. Na wala usisahau kamwe kwamba, hata kama utazikwa na kundi kubwa la watu wote wa dunia hii, lakini bado kaburini utabaki peke yako tu. Hakuna atakayekubali kubaki nawe milele! Kila mmojawao atarejea nyumbani kuendelea na harakati zake, akiwemo hata yule mpendwa wako saaaaaaaaaaaaana aliyekuwa akilia na kujigaragaza ovyo huku na kule kwa ajili ya kifo chako! Akili kichwani mwako.    

 

No comments: