MOJAWAPO YA MIRADI YA TASAF NDANI YA JAMII-WILAYANI ARUSHA...

Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Ilkiushin, Wilaya ya Arusha (Arusha Vijijini), Mh. William Samwel Kalama, akifungua rasmi Semina iliyofanyika hivi karibuni katika Kijiji chake, kwa kuwakaribisha wawezeshaji na wanasemina, wakati wa Semina juu ya mradi ulioibuliwa na wanakijiji wenyewe wa Kijiji cha Ilkiushin, mradi wa utengenezaji wa barabara, ambao unawezeshwa na TASAF.




Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Ilkiushin, Bwana Denis Mcharo, akiusikiliza kwa makini ukaribisho wa Mwenyekiti wa Kijiji chake, Mh. William Samwel Kalama, kwa wawezeshaji pamoja na wanasemina.




Humu ndimo Semina hii ilipofanyikia. Hili ni jengo la ofisi za Kijiji cha Ilkiushin.




Toilet ya Ofisi ya Kijiji….




Mmoja wa wawezeshaji wa Semina hii, kiongozi wa upembuzi shirikishi katika kuwezesha jamii kuibua miradi watakayoitekeleza wenyewe wakiwezeshwa, kwa kifupi EPRA, Bi. Zainabu Kivuyo, akielekeza na kuandika mambo muhimu ya msingi kwa kamati ya Kijiji, wakati itakapokuwa katika utekelezaji wa mradi.




Sehemu ya majukumu ya kamati ya Kijiji kwa mradi huo wa barabara….




Mwezeshaji mwingine, Bwana Jabir Ally, ambaye ni mratibu wa TASAF Wilaya ya Arusha (Arusha Vijijini), naye akiwa kazini ndani ya semina hii, akitoa maelekezo juu ya namna ya suala zima la umuhimu wa usimamizi wa mradi.




Mtaalamu wa masuala ya kifedha, Bwana Dixon Andindilile, ambaye ni mhasibu (Bwana fedha) wa TASAF wilaya ya Arusha (Arusha Vijijini), akiwa katika eneo lake la kitaaluma akiwapa mwongozo washiriki wa semina, katika namna na jinsi masuala mazima ya kifedha (uchukuaji na utumiaji) yanavyotakiwa kupangiliwa na kutunzwa kitaalamu kwa ajili ya ukaguzi pamoja na uhakiki. Hapa akiwaonesha washiriki wa Semina hii hundi ya fedha jinsi ilivyo, na namna ya matumizi yake katika mradi.





Washiriki wakiwasikiliza kwa makini wawezeshaji wao, na huku baadhi yao wakipewa nafasi ya kusimama na kuuliza maswali au kutaka kupewa ufafanuzi wa masuala pamoja na mambo mbalimbali ambayo yanawatatiza ama kutoeleweka vema kwa upande wao juu ya mradi mzima, wakati Semina ilipokuwa ikiendelea.

No comments: