UNAWEZA UKAJIKUTA UKIPATWA NA DAZENI NZIMA YA MASWALI TELE NDANI YA KICHWA CHAKO! LABDA HATA UNAWEZA UKAFIKIRI KWAMBA SIKU HIZI CHAMA KIMEANZISHA HUDUMA ZA UFUNDI KWENYE OFISI ZAKE; NA HAWA NI MAFUNDI WAKE WAKIWA KAZINI!


Wakijadiliana jambo fulani kabla ya kuanza kazi..



Haya, sasa, mwanamume kaza mikono; kamata vizuri! Haya, twende kazi...



Maswahiba; mafundi, Kitaringo, aliyeshika bomba mkononi, na mwenzake Kibakuli, wakiwa katika harakati za kutayarisha mabomba ya maji (wakiyawekea tred), tayari kwa kwenda kuyafunga kwenye nyumba ya mteja. Mpini Wa Shoka uliwanasa mafundi hawa wakiifanyia kazi yao hii nje ya Ofisi iliyokuwa imefungwa ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo-Tanzania (CHADEMA), kiasi ambacho unaweza ukadhani wao ni mafundi wa chama... 

No comments: