PAMOJA NA UPENZI MKUBWA ULIOZITEKA MNO NYOYO ZETU NYINGI KWA LIGI KUU MBALIMBALI ZA ULAYA KWA SOKA, LAKINI HATA NDANI YA MITAA NA VITONGOJI VYETU MBALIMBALI MABANGO KAMA HAYA KWA TIMU ZETU HUWA YANAONEKANA HAPA PALE...


Mpini Wa Shoka ulilinasa bango hili hivi karibuni kwenye viunga vya mtaa wa Jamhuri (Jaluo Street)-Daraja Mbili, Arusha. Ilikuwa ni mechi ya kirafiki ndani ya Jumapili moja hivi kati ya vijana wanaojishughulisha na  kazi ya ukusanyaji wa chuma chakavu (screpa) wa mtaa wa Jamhuri (Jaluo Street) Transcrap F.C dhidi ya Ngangu F.C. kwenye uwanja wa shule ya Sekondari Sinoni. Kwa mujibu wa mmoja wa washambuliaji hatari wa timu ya Transcrap, Fred, matokeo ya mechi hiyo yalikuwa ni: Transcrap 1 - Ngangu 0.

No comments: