VYOVYOTE VILE ULIVYOSHEREHEKEA; Mpini Wa Shoka UNAKUPA MKONO WA IDDI
Waislamu pande mbalimbali za Arusha, waliungana na waislamu wengine kote duniani katika kuisherehekea Sikukuu ya Idd El Fitri, baada ya kuikamilisha safari ya masiku machache tu (29 au 30) ya kuufunga (saumu) mwezi mtukufu wa Ramadhani. 
Baada ya sala ya Idd mapema asubuhi kwenye viwanja vya wazi na ndani ya misikiti, nyuso za tabasamu na furaha ndizo zilizotawala kila upande....
 Kukumbatiana kwa bashasha na mahaba kama hivi, ndiko kulikotawala zaidi
Kukumbatiana kwa bashasha na mahaba kama hivi, ndiko kulikotawala zaidi 
 Na kama kawaida, waheshimiwa wadogowadogo kama hawa iliwabidi wawe wakipatiwa msaada wa kuvalishwa viatu. Vinginevyo, uvaaji wao ulikuwa ni wa vihoja vitupu; kulia-kushoto, kushoto-kulia!
Na kama kawaida, waheshimiwa wadogowadogo kama hawa iliwabidi wawe wakipatiwa msaada wa kuvalishwa viatu. Vinginevyo, uvaaji wao ulikuwa ni wa vihoja vitupu; kulia-kushoto, kushoto-kulia! 
 Furaha na raha nyusoni kwa akina mama pia havikufichika hata kidogo
Furaha na raha nyusoni kwa akina mama pia havikufichika hata kidogo  
 Khadija Saidi Tilya (mwenye mtandio wa rangi ya zambarau) na Khadija Abdallah Chembe (aliyebeba mtoto), wakitoka msikitini kwenye sala ya Idd pamoja na waumini wengine. Anayewafuata nyuma ni Bi. Ashura.
Khadija Saidi Tilya (mwenye mtandio wa rangi ya zambarau) na Khadija Abdallah Chembe (aliyebeba mtoto), wakitoka msikitini kwenye sala ya Idd pamoja na waumini wengine. Anayewafuata nyuma ni Bi. Ashura. 
 Akbar Ally (mwenye kofia ya rangi nyeupe) na Rashid Omary katika pozi la picha ya Sikukuu ya Idd, kwenye msikiti uliopo eneo la Tanesco-Njiro
Akbar Ally (mwenye kofia ya rangi nyeupe) na Rashid Omary katika pozi la picha ya Sikukuu ya Idd, kwenye msikiti uliopo eneo la Tanesco-Njiro 
 Hapa ni Ramadhani Abdallah, Swalehe Rashid na Rashid Omary
Hapa ni Ramadhani Abdallah, Swalehe Rashid na Rashid Omary
 
 EID MUBARAK 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment